Diamond akanusha kuwalipisha pesa wanaotaka kumuona Tiffah uso kwa uso


Kwa umaarufu alionao mtoto wa Diamond na Zari, Latiffah Nasib Abdul au kama baba yake anavyopenda kumuita Tiffah, ni wazi kwamba mashabiki wengi wa staa huyo wangependa kumuona ama kumbeba mtoto huyo aliyejipatia umaarufu toka siku yake ya kwanza duniani.







Hiyo inatokana pia na uamuzi wa wazazi wake kutomuonesha mapema sura yake hadi Jumapili iliyopita, ambayo iliongeza shauku hiyo.

Licha ya kuwa picha za kwanza kuonesha sura zake zilidhaminiwa na makampuni, lakini Dimond amekanusha uvumi kuwa anatoza kiasi fulani cha fedha kwa watu wa kawaida ambao wangepeda kumuona Tiffah uso kwa uso. Diamond Ameiambia BBC kuwa habari hizo ni za uongo.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment