Linah: Nimeshatambulishwa kwa wakwe zangu Uganda
Linah anadai tayari ameshatambulishwa kwa wazazi wa mpenzi wake mpya ambaye ni raia wa Uganda, Williams Bugeme.
Hata hivyo Linah ameiambia Bongo5 kuwa sasa hivi wameamua kupunguza kujionyesha sana ili wapate muda wa kufanya kazi.
“Namshukuru Mungu mama mkwe alinipokea vizuri sana,” Linah ametuambia. “Wadogo zake pamoja na marafiki. Najivunia kuwa naye sema sasa hivi tumeamua tupunguze kujionyesha. Kama mapenzi yapo tu huu ni wakati wa kufanya kazi kwanza,” ameongeza.
Kwa upande mwingine Linah ambaye ni miongoni mwa wasanii waliotajwa kuwania tuzo za kimataifa za Afrima, amewataka watanzania kuunga mkono kazi zake pamoja na kumpigia kura.
0 comments:
Post a Comment