Wakati ambapo WWE ikijiandaa kwa ajili ya Royal Rumble 2016 na WrestleMania 32, mshindi wa mara 15, John Cena atafanyiwa upasuaji wa bega.
Cena ametangaza hatua hiyo kupitia Twitter, Alhamis hii.
'' Rather upside down start to 2016 as tomorrow I will head to Birmingham for shoulder surgery. Life's full of set backs but #nevergiveup
— John Cena (@JohnCena) January 7, 2016
Kumkosa Cena litakuwa pigo kubwa kwa WWE ambayo tayari wachezaji mieleka wake wengi ni majeruhi wakiwemo Daniel Bryan, Sting, Randy Orton, Seth Rollins, Cesaro na wengine.
Hata hivyo wana mieleka wakongwe wakiwemo The Undertaker, The Rock na Brock Lesnar watasaidia kuziba pengo la Cena kama hatoweza kushiriki kwenye WrestleMania 32.
Wachambuzi wa mchezo huo wamedai kuwa ni muda wa WWE kutengeneza staa mwingine huku Roman Reigns akionekana kuwa kipenzi kipya cha wengi.
0 comments:
Post a Comment