Katy Perry awa mtu wa kwanza kufikisha followers milioni 80 Twitter
Muimbaji Katy Perry, ameuanza vyema mwaka mpya kwa kuweka rekodi mpya ya kuwa mtu wa kwanza kuwahi kufikisha followers milioni 80 kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter.
Katy Perry ambaye hivi sasa ana followers milioni 80.4 anafatiwa na Justin Bieber mwenye followers milioni 72.9 na wa tatu ni Taylor Swift ambaye ana followers milioni 68.8.
Anaamini kuwa amefanikiwa kuwa na followers wengi kiasi hicho kutokana na kutweet mwenyewe.
“’I would say 90 per cent of my Tweets, I’ve just made them up and you can tell because many of them are misspelled and full of typos” alisema Katy.
Mwaka 2015 pia Katy Pery alitajwa na jarida la Forbes kuwa staa aliyeingiza fedha nyingi zaidi kwa mwaka jana pekee, kiasi cha dola milioni 135.
0 comments:
Post a Comment