Wachezaji wa klabu ya Manchester City Joe Hart na Raheem Sterling watakosa mechi za kirafiki za England dhidi ya Germany na Holland baada ya nyota hao wawili kuumia na kutolewa katika mchezo wao na Manchester United.

Joe Hart aliumia mguu wake wa kulia katika harakati za kumuwahi Anthony Martial asifunge baada ya pasi mbovu ya nyuma kutoka kwa beki Martin Demichelis na Sterling alitolewa kipindi cha kwanza baada ya kugongana na Juan Mata.

Kwa mujibu wa kocha wa City, Manuel Pellegrini amesema nyota hao watakuwa nje kwa mwezi mmoja na kukosa mechi za maandalizi ya Timu ya Taifa kwaajili ya Euro 2016, ambapo England itajipima nguvu na Ujerumani huko Berlin Jumamosi ijayo kabla ya kurejea Wembley kuikabili Holland siku tatu baadae.
0 comments:
Post a Comment