Nick wa Pili amedai kuwa imani kwamba wasanii hujiingiza kwenye matumizi ya madawa ya kulevya kwasababu ya stress za maisha si za kweli.
Amedai kuwa stress ni kitu kinachowapata watu wengi si wasanii tu.
“Maisha tunayoishi watu wengi sana tuna stress hatuwezi kusema sisi wanamuziki tuko special, watu wako stressed a lot lakini mbona hawali unga?” alihoji Nick kwenye kipindi cha Ladha 3600 cha EFM.
Nick alidai kuwa vijana wanatakiwa kuepuka kabisa na matumizi ya vitu kama bangi au vilevi vikali ambavyo huwapelekea kuingia kwenye matumizi ya madawa ya kulevya.
0 comments:
Post a Comment