Jokake apagawishwa na Alikiba!



NYOTA wa muziki wa kizazi kipya nchini, Jokate Mwegelo, amemsifu msanii mwezake Ali Salehe ‘Ali Kiba’ kwa kutumbuiza muziki na ‘live Band’ kitu kinachoongeza mvuto kwenye maonyesho yake.

Akizungumza na MTANZANIA, Jokate alisema Ali Kiba ni mfano wa kuigwa kwa sababu muziki unakua na soko la kimataifa linahitaji wasanii wanaotumia ala za muziki wawapo jukwaani.

“Ali Kiba ni mfano wa kuigwa, wasanii tusipende kutumia CD kwenye majukwaa tunadumaza vipaji vyetu ni vyema tukafahamu mashabiki pia wamechoka mtindo wa ‘Play Back’,” alisema Jokate.

Aliongeza kuwa alishawishika kuhudhuria onyesho la Funga Mwaka na Ali Kiba kwa sababu alijua burudani inayotolewa na msanii huyo huwa ni ‘live’ kwa kutumia ala za muziki.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment