Nyumba mbili za Wastara kupitiwa na bomoa bomoa


Muigizaji wa filamu, Wastara Juma amejikuta katika wakati mgumu tena baada ya nyumba zake mbili kupitishiwa X kwaajili ya kubomolewa siku zijazo.


Katika ukurasa wake wake wa Facebook, Wastara ameandika:

Mashabiki wangu mwaka umeanza vibaya kwangu nyumba zangu mbili zimewekwa X na zitabomolewa siku yoyote kuanzia leo,siko sawa kabisa niombeeni dua presha imepanda,nawapenda sana

Akiongea na Bongo5, ndugu wa Wastara amethibisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa hali ya muigizaji huyo si nzuri kutokana na mshtuko alioupata.

“Kweli Wastara hali yake sio nzuri amepata mshtuko baada ya watu wa mazingira kuweka X katika nyumba zake mbili,” alisema dada huyo aliyejitambulisha kwa jina la Mariam uku akidai Wastara hawezi kuongea na simu.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment